Mwanafunzi wa darasa la Herieth Kitunduru
akiwakumbusha masomo wanafunzi wa darasa la tano leo baada ya walimu
kugoma
Mkuu wa shule ya Mtwivila Christabela Alfani ambaye
ametelekezewa shule ya walimu wenzake leo
Wanafunzi wa darasa la saba shule ya Msingi Kihesa
wakiendelea kufundishwa leo baada ya walimu wao kugomea mgomo wa walimu
Mkuu wa shule ya msingi Kihesa Zabihu Hassan akiwa
kazini
Mwalimu wa shule ya Msingi Kihesa akiendelea na kazi leo
hivi ndivyo walivyofanya walimu wa Mtwivila Iringa
kwa kujiorodhesha bila kuwepo kazini
Wanafunzi wa darasa la tano
Mkuu wa shule ya Msingi Wilolesi Gabriel Kameka
akiendelea na kazi kama kawaida
Wapiganaji wa al-Shabab
Mmarekani aliyetuhumiwa kwa kujaribu kujiunga na kundi lenye
msimamo mkali la Kiislam la al-Shabab nchini Somalia amekiri mashtaka yake
kwenye mahakama Marekani.
Shaker Masri, 28, alikamatwa Agosti 2010 akijiandaa kusafiri kwenda Somalia
kukijunga na al-Shabab, kwa mujibu wa mwendesha mashtaka wa Marekani.Katika makubaliano ya kukubali mashtaka, Masri amekubali kutumikia kifungo chini ya miaka kumi gerezani.
Alikiri kupanga njama za kukusanya fedha alizohitaji kujzitumia katika jihadi ama Somalia au Afghanistan.
Amehukumiwa kifungo za miaka 15 gerezani.
Masri alizaliwa Alabama na kuishi Chicago kabla ya kukamatwa saa chache hajaondoka nchini.
Amekuwa akijieleza kama wakala wa FBI wa siri na amekuwa akizungumzia kuhusu kuwalenga ‘makafiri’
Kufuatia kukamatwa kwake alishtakiwa kwa kujaribu kusaidia kwa mali kundi la kigaidi, akijaribu kuwapa msaada kwa kutumia silaha za maangamizi.
Taarifa kamili za kukiri kwake hazijatolewa kwa umma.
Al-Shabab wanaamini kuwa ikiwapata wasomali wenye asili ya Kimarekani kushiriki katika kujitoa muhanga nchini Somalia na maafisa wa Marekani sasa wana wasiwasi wa kuwepo shambulio ndani ya Marekani.
Raia kadhaa wa Marekani wamekamatwa katika miaka ya karibuni wakijaribu kushiriki au kuunga mkono vita vya zaidi ya miongo miwili iliyopita.
Shaker Masri atahukumiwa rasmi mwezi Oktoba 16.





















